NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

UJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, ukiongozwa na mwenyekiti wake, Mhe. Mihayo Juma Nunga umetembelea ofisi za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) jijini Dar es Salaam hivi karibuni kwa nia ya kubainisha masuala muhimu ya Fidia kwa Wafanyakazi.

Akizungumza baada ya kukutana na Watendaji wa WCF wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Dkt. John Mduma, Mwenyekiti huyo amesema ziara hiyo imewawezesha kupata uelewa mpana wa namna Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi inavyotekelezwa.

“Kwetu jambo hili ni geni bado halijatengenezewa utaratibu bora zaidi wa kuwalipa fidia wafanyakazi waliopata changamoto kwenye maeneo ya kazi, Zanzibar tuko katika maandalizi ya kutengeneza utaratibu wa jinsi gani Mfanyakazi atapata fidia pindi anapoumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi, kwahivyo tukaona tutembelee Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ambao wana uzoefu mkubwa katika masuala haya.” Alifafanua Mhe. Nunga.

Alisema wameona jinsi watu wengi walivyonufaika na uwepo wa WCF kwa hivyo ni wakati muafaka kwa Zanzibar kuwa na Mfuko utakaotoa huduma bora kama ambavyo wameshuhudia hapo WCF.

Naye Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Bw.Ali Nassor Shaaban, alisema Mfuko huo uko katika maandalizi ya kuanzisha huduma kama hiyo ya kufidia wafanyakazi wanaoumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi.

“Tumeona kabla ya kuanzisha chombo hicho ni vema kujifunza kwa wenzetu WCF ili kujua sheria na kanuni zake zilivyo ili tuwe katika nafasi nzuri ya kuanzisha chombo chetu kitakachotoa huduma kulingana na mazingira ya Zanzibar.” Alifafanua.m

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dtk. John Mduma amesema , WCF ina uzoefu wa miaka saba (7) katika masuala ya utoaji fidia kwa wafanyakazi na imekuwa ni wakati mzuri wa kubadilishana mawazo ya namna bora ya kuendesha vyombo hivi vya Fidia kwa Wafanyakazi.

“Tumewaeleza namna tunavyotenda katika miaka hii saba (7) na tumejifunza mambo mengi ambayo wamekuwa wakituuliza na tunaamini wamejifunza mengi.” Alifafanua.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mihayo Juma Nunga (kushoto), akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dtk. John Mduma (kulia) na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Bw. Ali Nassor Shaaban wakati wa ziara ya Kamati hiyo na watendaji wa ZSSF kwenye Ofisi za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ili kujifunza jinsi unavyoendesha shughuli zake hususan ulipaji fidia kwa wafanyakazi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mihayo Juma Nunga (kulia), akizungumza mbele ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dtk. John Mduma wakati wa ziara ya kamati hiyo na watendaji wa ZSSF kwenye ofisi kuu za WCF jijini Dar es Salaam. 

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dtk. John Mduma (kushoto), akizungumza mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mihayo Juma Nunga wakati wa ziara ya ujumbe wa kamati hiyo na watendaji wa ZSSF kwenye ofisi za WCF jijini Dar es Salaam Oktoba 12, 2022
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Bw.Ali Nassor Shaaban, akifurahia jambo wakati wa mazungumzo na watendaji wa WCF.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati wakifuatilia elimu iliyokuwa ikitolewa na wataalamu wa WCF kuhusu masuala ya fidia kwa wafanyakazi
Baadhi ya wajumbe wa Kamati wakifuatilia elimu iliyokuwa ikitolewa na wataalamu wa WCF kuhusu masuala ya fidia kwa wafanyakazi
Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omar, akifafanua kuhusu namna Mfuko unavyofanya tathmini ya madhara aliyopata Mfanyakazi kutokana na ulemavu uliosababishwa na ajali iliyotokana na kazi.
Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw. Anselim Peter akifafanua kuhusu wajibu wa mwajiri katika kujisajili na kuwasilisha michango kwenye Mfuko.
Mkuu wa Huduma za Sheria WCF, Bw. Abraham Siyovelwa, akizungumzia Sheria iliyoanzisha Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF).
Meneja Mipango na Utafiti WCF, Bw. Patrick Ngwila akizungumzia masuala mbalimbali yanayohusu utendaji wa Mfuko
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Sheria Ndogo ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mihayo Juma Nunga (wakwanza kushoto) na ujumbe wake wakisikiliza kwa makini.














Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...