Mamlaka
ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imetambulisha mfumo wa Usajili wa Watu
kwa njia ya Mtandao (Online Registration) utakaowezesha Wananchi wenye
sifa za kuomba Vitambulisho vya Taifa kwa Kujaza fomu mtandao mahali
popote walipo bila kulazimika kwenda Ofisi za Usajili za Wilaya au vituo
vya Usajili wa NIDA.
Akizungumza
na Waandishi wa Habari leo Desema 21,2022 jijini Dar es Salaam Kaimu
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano NIDA, Geofrey Tengeneza amesema ili
kujisajili kwa njia ya mtandao Mwombaji ataandika eonline.nida.go.tz katika mtandao wa internet na kufuata maelekezo.
"Mfumo
huu unalenga kupunguza usumbufu kwa Woambaji wa Vitambulisho vya Taifa
ambao kwa sasa wanalazimika kufika Ofisi za NIDA kuchukua fomu za maombi
ya Vitambulisho vya Taifa kwani kupitia mfumo huu ujazaji wa fomu na
kuweka viambatisho utafanyika mahali popote kwa kutumia kifaa chenye
uwezo wa kupokea mtandao wa Mawasiliano (Intaneti)" ,amesema Tengeneza.
Amesema
kuwa baada ya kujaza fomu mwombaji atatakiwa kuchapa fomu (print) na
kuipeleka serikali ya Mtaa anapoishi kwa ajili ya kuthibitisha ukaazi
wake kisha atatakiwa kupeleka fomu yake ofisi ya NIDA iliyoko katika
Wilaya anayoishi akiwa na nakala ngumu za viambatisho alivyopakia katika
mfumo ili kukamilisha utaratibu wa usajili kama vile kuhojiwa na
Uhamiaji,kupigwa picha na kuchukuliwa alama za vidole.
Tengeneza
amefafanua kuwa mfumo huo utapunguza muda unaotumika katika kusajili
taarifa za mwombaji kwa kuwa usajili wa taarifa za mwombaji utakuwa
umefanywa na Mwombaji mwenyewe.
"Pamoja
na kurahisisha huduma ya usajili kwa Raia na Wageni Wakaazi,utapunguza
pia gharama zinazotumika katika kuchapisha fomu za usajili na gharama za
uchakataji wa taarifa",amesema Tengeneza
Amesema
kuwa usajili kwa njia ya Mtandao utaongeza idadi ya Watu wanaojisajili
kwa kuwa huduma hiyo itapatikana mahali popote badala ya kufika katika
ofisi Ya NIDA kufuata huduma hiyo.
Kwa
upande wake Meneja Usajili na Utambuzi (NIDA), Bi.Julien Mafuru amesema
kumekuwa na malalamiko ya kukosewa kwa taarifa za uombaji vitambulisho
hivyo kupitia mfumo huu utasaidia kupunguza kero hiyo kwani mwombaji
atajaza taarifa zake mwenyewe.
Amesema
wanaenda kupanua wigo wa kuwaandikisha watanzania ambao watakuwa nje ya
nchi kwahiyo na wenyewe watapata faida ya kujaza foma moja kwa moja
kwenye mtandao.Kaimu
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa
(NIDA) Bw.Geofrey Tengeneza akifafanua zaidi mbele ya waandishi wa
habari leo Desemba 21,2022 katika ofisi za NIDA Jijini Dar es Salaam
namna ya kujisalijili mtandaoni ili kupata kitambulisho cha Taifa.
Kaimu
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa
(NIDA) Bw.Geofrey Tengeneza (katikati) akizungumza na waandishi wa
habari leo Desemba 21,2022 Jijini Dar es Salaam, kushoto kwake ni Meneja
Usajili na Utambuzi (NIDA), Bi.Julien Mafuru na kulia kwake ni Kaimu
Mkuu Uratibu Ofisi za Wilaya NIDA, Bi.Brenda Kileo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...