Benki Kuu ya Tanzania imeibuka mshindi wa kwanza katika kipengele cha ‘Uzingatiaji wa Sheria, Miongozo na Kanuni za Serikali Mtandao’.

Tuzo hiyo kwa BOT imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma, Mhe. Deogratius Ndejembi, tarehe 8 Februari 2023 jijini Arusha kwenye kikao kazi cha 3 cha Serikali Mtandao kilichoandaliwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA).

Kikao kazi hicho kimewakutanisha watumishi wa umma na wadau wengine kutoka taasisi mbalimbali za Serikali kujadili juu ya mafaniko na changamoto za utekelezaji wa serikali mtandao (matumizi ya TEHAMA serikalini) kikiwa na kauli mbiu ya “Mifumo Jumuishi ya TEHAMA kwa utoaji bora wa huduma za umma”.

Aliyepokea tuzo hiyo kwa niaba ya Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania ni Meneja Idara ya Uundaji na Usimamizi wa Mifumo, Bw. Christopher Nyato.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...