Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akisaini kitabu cha Wageni katika Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza, ambako anafanya ziara ya kikazi kwa ajili ya majadiliano na Viongozi wa Taasisi za Kimataifa na baadhi ya viongozi waandamizi wa Serikali ya Uingereza kwa ajili ya Mipango ya maendeleo ya Tanzania.


Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), (katikati) akingalia jambo kuhusu miundombinu yaJengo la Ubalozi, kwenye simu ya Mwambata wa Kijeshi- Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza, Brigedia Jenerali Bright Msuya (kushoto). Kulia ni Balozi wa Tanzania- Uingereza Dkt. Asha-Rose Migiro, wakati mstari wa nyuma, kushoto ni Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Madeni Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Japhet Justine, Kamishna wa Fedha za Nje Bw. Rished Bade na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mali za Serikali Bw. Chotto Sendo, Jijini London nchini Uingereza

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa Tanzania pamoja na maafisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza ambako anafanya ziara ya kikazi. Kushoto kwa Mhe. Waziri ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango-Zanzibar Dkt. Juma Malik Akil, Mwambata Fedha, Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza, Bi. Anath Lwenduru, na kulia kwake ni Balozi wa Tanzania- Uingereza Dkt. Asha-Rose Migiro, Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Madeni Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Japhet Justine.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WFM, London,Uingereza)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...