NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma (wa pili kushoto) na Mkuu wa Wateja Wakubwa na Serikali wa benki ya NBC, James Meitaron (wa pili kulia) wakimkabidhi kombe mshindi wa kwanza wa mashindano ya NBC Lugalo Open 2023 Ally Mcharo kutoka klabu ya TPC, Kilimanjaro katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya Jeshi vya Gofu Lugalo, Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Mwenyekiti wa klabu ya Lugalo, Brigedia Generali mstaafu Michael Luwongo na Rais wa TLGU, Queen Siraki
 Mwenyekiti Wa Klabu ya Lugalo Gofu Brigedia Jenerali Mstaafu Michael 
Luwongo (katikati),Katibu wa Klabu hiyo, Luteni Kanali Shabani 
Kitogo(Kulia)na Meneja Masoko wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC, Alina 
Maria Kimaryo (wapili kushoto) wakikabidhi zawadi ya baiskeli kwa 
mshindi wa kwanza upande wa watoto (Juniors) katika Shindano la "NBC 
Lugalo Open 2023" , Omari Shabani. Kutoka kushoto ni Msimamizi wa 
Mashindano wa Chama Cha Mchezo wa Gofu Tanzania TGU, Ernest Sengeu.
 Mwenyekiti Wa Klabu ya Lugalo Gofu Brigedia Jenerali Mstaafu Michael 
Luwongo (katikati),Katibu wa Klabu hiyo, Luteni Kanali Shabani 
Kitogo(Kulia)na Meneja Masoko wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC, Alina 
Maria Kimaryo (wapili kushoto) wakikabidhi zawadi ya baiskeli kwa 
mshindi wa kwanza upande wa watoto (Juniors) katika Shindano la "NBC 
Lugalo Open 2023" , Omari Shabani. Kutoka kushoto ni Msimamizi wa 
Mashindano wa Chama Cha Mchezo wa Gofu Tanzania TGU, Ernest Sengeu. NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma akicheza 
mchezo wa Gofu katika kufunga mashindano ya NBC Lugalo Open 2023 katika 
hafla iliyofanyika katika viwanja vya Jeshi vya Gofu Lugalo, Dar es 
Salaam mwishoni wa wiki iliyopita wanaoshuhudia ni kulia ni Mkuu wa 
Wateja Wakubwa na Serikali wa benki ya NBC, James Meitaron na kulia ni 
Mwenyekiti wa klabu ya Lugalo, Brigedia Generali mstaafu Michael Luwongo
 .
 NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma akicheza 
mchezo wa Gofu katika kufunga mashindano ya NBC Lugalo Open 2023 katika 
hafla iliyofanyika katika viwanja vya Jeshi vya Gofu Lugalo, Dar es 
Salaam mwishoni wa wiki iliyopita wanaoshuhudia ni kulia ni Mkuu wa 
Wateja Wakubwa na Serikali wa benki ya NBC, James Meitaron na kulia ni 
Mwenyekiti wa klabu ya Lugalo, Brigedia Generali mstaafu Michael Luwongo
 .  Dar es Salaam, Tanzania: Machi 27, 2023 - Naibu Waziri wa Utamaduni, 
Sanaa, na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma ameipongeza Benki ya NBC kutokana
 na jitihada zake za kusaidia maendeleo ya michezo mbali mbali nchini.
 Dar es Salaam, Tanzania: Machi 27, 2023 - Naibu Waziri wa Utamaduni, 
Sanaa, na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma ameipongeza Benki ya NBC kutokana
 na jitihada zake za kusaidia maendeleo ya michezo mbali mbali nchini.  Akizungumza wakati hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa mchezo wa 
gofu wa NBC Lugalo Open 2023 iliyofanyika katika viwanja vya Jeshi 
Lugalo jana, Mh. Mwinyijuma alisema benki ya NBC imekuwa ikitoa mchango 
mkubwa katika sekta michezo hapa nchini na kuongeza kuwa Serikali 
inatambua mchango wa benki hiyo. “Nikiwa kama Naibu Waziri mwenye 
dhamana ya Utamaduni, Sanaa, na Michezo napenda kuishukuru benki ya NBC 
kwa kutuunga mkono katika jitihada za kuendeleza na kukuza maendeleo ya 
michezo.
 Akizungumza wakati hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa mchezo wa 
gofu wa NBC Lugalo Open 2023 iliyofanyika katika viwanja vya Jeshi 
Lugalo jana, Mh. Mwinyijuma alisema benki ya NBC imekuwa ikitoa mchango 
mkubwa katika sekta michezo hapa nchini na kuongeza kuwa Serikali 
inatambua mchango wa benki hiyo. “Nikiwa kama Naibu Waziri mwenye 
dhamana ya Utamaduni, Sanaa, na Michezo napenda kuishukuru benki ya NBC 
kwa kutuunga mkono katika jitihada za kuendeleza na kukuza maendeleo ya 
michezo. NBC imekuwa ikifadhili michezo mbali mbali kiwa ni pamoja na ligi ya Kuu ya Tanzania bara, Dodoma Marathon n.k. Ligi yetu kwa sasa ni moja ya ligi zinazotajwa kuwa ni ligi bora barani Afrika na hii imewezekana kutokana na mchango wabenki ya NBC,” alisema Mhe. Mwinjuma. Aliongeza: “Ni rai yangu kwa NBC kuendeleza kuweka mkono kwenye michezo yetu na kwenye sehemu nyingine za kijamii hapa nchini.
Makampuni na taasisi nyingine pia ziige wanachokifanya benki ya NBC ili tuweze kupiga hatua kubwa na kwa haraka zaidi,” Naibu Waziri aliipongeza NBC kufadhili michezo mbali mbali “Sikutegemea kuwakuta kwenye gofu, nimefurahishwa na jitihada zenu kwa kuwa mstari wa mbele katika kukuza na kuimarisha michezo Tanzania. Hongereni sana NBC nyinyi ni mfano wa kuigwa,” aliongeza Mhe. Mwinjuma.
 Aidha, Mkuu wa Wateja Wakubwa na Serikali wa benki hiyo Bw. James 
Meitaron alisema kuwa kupitia sera ya kurudisha kwa jamii, benki hiyo 
itaendelea kuunga mkono jitihada za serikali kuendeleza na kukuza 
michezo mbali mbali nchini. “Tunaamini kuwa ushiriki wetu kwenye eneo 
hili la michezo pamoja na kusaidia juhudi za serikali katka maeneneo 
mengine, utasaidia kuboresha maisha ya Wanzania ikiwa pia ni sehemu yetu
 ya kurudisha kwa jamii . Kama tulivyoahidi hapo awali, leo tumetoa tuzo
 mbali mbali kwa washiriki wa mashindano haya ya wazi ya NBC Lugalo 2023
 yaliyoanza jana,” alisema Bw. Meitaron.
 Aidha, Mkuu wa Wateja Wakubwa na Serikali wa benki hiyo Bw. James 
Meitaron alisema kuwa kupitia sera ya kurudisha kwa jamii, benki hiyo 
itaendelea kuunga mkono jitihada za serikali kuendeleza na kukuza 
michezo mbali mbali nchini. “Tunaamini kuwa ushiriki wetu kwenye eneo 
hili la michezo pamoja na kusaidia juhudi za serikali katka maeneneo 
mengine, utasaidia kuboresha maisha ya Wanzania ikiwa pia ni sehemu yetu
 ya kurudisha kwa jamii . Kama tulivyoahidi hapo awali, leo tumetoa tuzo
 mbali mbali kwa washiriki wa mashindano haya ya wazi ya NBC Lugalo 2023
 yaliyoanza jana,” alisema Bw. Meitaron.  Kwa upande, mshindi wa kwanza wa mashindano hayo Bw. Ally Mcharo 
aliishukuru benki ya NBC kwa kudhamini na kufanikisha mashindano na pia 
aliushukuru uongozi wa Klabu ya Gofu ya Lugalo kwa kukubali kufanya 
mashindano hayo na kuwapa fursa vijana kuweza kuonyesha vipaji vyao.
 Kwa upande, mshindi wa kwanza wa mashindano hayo Bw. Ally Mcharo 
aliishukuru benki ya NBC kwa kudhamini na kufanikisha mashindano na pia 
aliushukuru uongozi wa Klabu ya Gofu ya Lugalo kwa kukubali kufanya 
mashindano hayo na kuwapa fursa vijana kuweza kuonyesha vipaji vyao. 
 
 





 

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...