Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano wa kibiashara na uwekezaji baina yake na Marekani na inawakaribisha wawekezaji kutoka nchini humo kuja kuwekeza na kushirikiana na watanzania katika ufanyaji biashara katika sekta mbalimbali nchini.
Dkt. Kijaji ameyasema hayo alipokutana na 
kufanya mazungumzo kuhusu kuendeleza uhusiano wa kibiashara na uwekezaji
 baina ya nchi hizo na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Michael Battle 
Machi 27, 2023 katika Ofisi ndogo ya Wizara, jijini Dar es Salaam.
Aidha,
 Waziri Kijaji ameiomba Marekani kuongeza muda wa Mkataba wa Mpango wa 
Ukuzaji fursa za Kiuchumi Afrika (AGOA) uliotiwa saini mwaka 2000 na 
awamu inayotarajiwa kuisha ni kati ya 2015 na 2025. 
Akifafanua 
zaidi, Dkt. Kijaji amesema Mpango huo wa AGOA unalenga kutoa fursa ya 
upendeleo kwa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara kupeleka bidhaa 
zaidi ya 6,500 bila kulipa ushuru wa forodha nchini Marekani 
 
Dkt. Kijaji pia ameainisha kuwa Tanzania ni moja ya nchi inayonufaika na
 fursa ya Mpango wa AGOA ambapo Sekta ya Nguo na Mavazi inachangia mauzo
 kwa asilimia 95. Kutoka katika Viwanda vikubwa vya Mazava Fabrics and 
Production E.A L, na Tanzania Tooku Garments Co., Ltd . Bidhaa zingine 
zinazochangia asilimia 5 ni bidhaa za Mikono, Uchakataji bidhaa za 
kilimo (Agro-processing) na Ngozi.
Naye Balozi wa Marekani nchini
 Tanzania Mhe. Michael Battle amesema Marekani itaimarisha uhusiano wa 
kibiashara na uwekezaji na Tanzania hususani katika sekta mbalimbali 
ikiwemo viwanda na kufanya biashara na benki za kitanzania ili 
kirahisisha upatikanaji wa mitaji kwa wafanyabiashara wa Tanzania.


 

.jpeg)

.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...