Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiwasalimu waumini waliohudhuria Ibada Ibada ya Jumapili katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro iliopo Swaswa Jijini Dodoma leo tarehe 16 Aprili 2023.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango na Mkewe Mama Mbonimpaye Mpango wakishiriki Ibada ya Jumapili katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro iliopo Swaswa Jijini Dodoma leo tarehe 16 Aprili 2023.
******

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa watanzania kuacha tabia ya kutupa taka ovyo katika maeneo mbalimbali wanayotumia hususani barabarani.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akiwasalimu waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro iliopo Swaswa Jijini Dodoma mara baada ya kushiriki Ibada ya Jumapili katika kanisa hilo leo tarehe 16 Aprili 2023.

Amesema uwepo wa mvua zisizotabirika ni kutokana na uharibifu wa mazingira uliokwishafanyika hivyo kila mmoja aone umuhimu wa utunzaji mazingira mazuri ambayo nchi imejaaliwa na Mwenyezi Mungu.

Makamu wa Rais ametoa rai kwa waumini hao na watanzania kwa ujumla kuona umuhimu wa kupanda miti katika makazi yao ikiwemo miti ya matunda na kivuli pamoja na kuongeza jitihada katika usafi wa mazingira ili kukabiliana na athari zitokanazo na uharibufu wa mazingira zinazojitokeza hivi sasa.

Halikadhalika Makamu wa Rais amewakumbusha waumini juu ya kuzingatia maadili mema ya kitanzania katika malezi ya watoto na vijana pamoja na kutoa wito kwa wamiliki wa taasisi za kutolea elimu kujielekeza katika kusimamia maadili mema ya kitanzania katika maeneo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...