Benki ya Stanbic na UNDP Tanzania wametangaza ushirikiano wenye lengo la kuimarisha upatikanaji wa mtaji na huduma za maendeleo ya biashara kwa kampuni changa na biashara ndogo na kati za Kitanzania.
Ushirikiano huu, chini ya mipango yao ya 
Stanbic Biashara Incubator na Funguo Innovation Programme, unalenga 
kuboresha ubora wa huduma za maendeleo ya biashara zinazotolewa na watoa
 huduma tofauti na waendeshaji wa uvumbuzi kwa kampuni na biashara 
changa zinazoongozwa na vijana na wanawake. Vilevile, unalenga kukuza na
 kusaidia mazingira yatakayoruhusu kampuni hizi kustawi.
Kadhalika,
 ushirikiano huu unalenga kutoa mafunzo ya kiufundi, na kujenga uhusiano
 na wawekezaji na wafadhili na kuongeza fursa kwa kampuni changa na 
biashara ndogo na kati ili kuongeza vyanzo mbalimbali vya mtaji. 
Utiaji
 Saini wa hati ya makubaliano, yaani Memorandum of Understanding 
ulifanyika kwenye hafla fupi iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa 
ubunifu na ujasiriamali, kutoka sekta ya umma, sekta binafsi, wadau wa 
maendeleo, waanzilishi wa kampuni za kibunifu pamoja na wandishi wa 
habari.
 Kusainiwa kwa hati hii kuliashiria kuanza rasmi kwa 
ushirikiano huo na kuanza kwa shughuli ya kwanza ya pamoja, ambayo 
ilihusisha mafunzo ya siku mbili juu ya mbinu na maarifa ya kutafuta 
mitaji ya uwekezaji kwa kampuni changa na biashara ndogo na za kati.
Ushirikiano
 huu unaendana na Lengo la 17 la Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja 
wa Mataifa, ambalo linasisitiza ushirikiano kwa maendeleo endelevu. UNDP
 Tanzania na Benki ya Stanbic Tanzania wanatambua kuwa ushirikiano ni 
muhimu katika kuendeleza mfumo wa uvumbuzi na ujasiriamali wa 
Kitanzania, na wamejitolea kufanya kazi pamoja kukuza maendeleo endelevu
 kupitia ushirikiano.
Akizungumza juu ya ushirikiano huu, Bi. 
Christine Musisi, Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania, alisema, 
"Tunafurahi kushirikiana na Benki ya Stanbic Tanzania kukuza ubunifu na 
ujasiriamali nchini Tanzania. 
Tunaamini ushirikiano huu 
utatusaidia kuongeza ufikiaji wa mtaji na huduma za maendeleo ya 
biashara kwa kampuni changa na biashara ndogo na kati za Kitanzania, 
hivyo kutengeneza fursa za ajira kwa vijana wa Kitanzania, na hatimae 
kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi."
Vivyo hivyo, Bw. Kevin 
Wingfield, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Stanbic Tanzania, alisema, 
"Tunafurahi kushirikiana na UNDP Tanzania kwenye mpango huu. Kama benki,
 tumejitolea kuunga mkono wajasiriamali na biashara ndogo ndogo, na 
tunaamini kuwa ushirikiano huu utasaidia sana kuongeza ufikiaji wa mtaji
 na huduma za maendeleo ya biashara kwa kampuni changa na biashara ndogo
 ndogo na kati za Kitanzania.”
 
Mwakilishi
 Mkazi wa UNDP Bi, Christine Musisi (Wapili kushoto) na Mkurugenzi 
Mtendaji wa benk ya Stanbic Tanzania Bw Kevin Wingfield (Wapili Kulia) 
wakisaini mkataba wa makubaliano ya kushirikiana katika kuimarisha 
upatikanaji wa mitaji na mafunzo ya kuwawezesha wafanyabiashara 
waanzishaji,wakati na wadogo kukuza biashara zao kupitia programu ya 
UNDP Funguo na Stanbic Biashara Incubator. Pichani  kulia ni  Mkuu wa 
kitengo cha StanbicBiashara Incubator  Kai Mollel na kushoto ni Meneja 
Mradi wa programu ya Funguo Joseph Maniraliza 
 
Mwakilishi
 Mkazi wa UNDP Bi, Christine Musisi (Wapili kushoto) na Mkurugenzi 
Mtendaji wa benk ya Stanbic Tanzania Bw Kevin Wingfield (Wapili Kulia) 
wakikabidhiana mkataba wa makubaliano ya kushirikiana katika kuimarisha 
upatikanaji wa mitaji na mafunzo ya kuwawezesha wafanyabiashara 
waanzishaji,wakati na wadogo kukuza biashara zao kupitia programu ya 
UNDP Funguo na Stanbic Biashara Incubator. Pichani kulia ni Mkuu wa 
kitengo cha Stanbic Biashara Incubator Kai Mollel na kushoto ni Meneja 
Mradi wa programu ya Funguo Joseph Maniraliza
 


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...