Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Dodoma

BOHARI ya Dawa (MSD) imeanika hatua mbalimbali inazochukua kuondokana na changamoto ya kuagiza vifaa tiba mbalimbali kutoka nje ikiwa pamoja na kuanzisha viwanda viwili vya barokoa na kimoja cha kuzalisha mipira ya mikono (groves).

Hayo yamesemwa leo Aprili 6, 2023 na Hassan Ibrahimu kutoka Idara ya Mipango, Tathimini na Ufuatiliaji wa Bohari ya Dawa (MSD), alipokuwa akielezea sababu za bohari hiyo kuanzisha kampuni tanzu na viwanda vyake.

Akifafanua zaidi wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari nchini katika semina iiyoandaliwa na MSD kuwajengea uwezo kuhusu shughuli za za bohari hiyo, Ibrahim amesema moja ya kiwanda kinachomilikiwa na MSD ni kinachozalisha barakoa kilichopo Keko jijini Dar es Salaam.

“Kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha barakoa 80 kwa dakika, uwekezaji wake ni Sh. bilioni 1.4 ambacho kwa mwaka kinazalisha barakoa milioni 5.8 kilianza kazi Agosti 2020. Kiwanda hiki kinaonesha umuhimu wa viwanda, kilianza kazi wakati wa janga la UVIKO-19 na wakati ule haikuwa rahisi kupata barakoa.

“Barakoa moja ilikuwa ikiuzwa sh. 1,600 lakini baada ya kiwanda kuja sasa inauzwa Sh. 500, uwepo wa kiwanda hiki umesaidia kabisa kuacha kuagiza nje, kwa maana hiyo kiwanda kimepunguza matumizi ya fedha za kigeni,” amesema Ibrahim.

Pia, amesema kiwanda kingine ni cha kuzalisha barakoa za N95 chenye uwezo wa kuzalisha barakoa 100 hadi 150 kwa saa moja ambacho kimekamilika na kuzinduliwa rasmi Machi mwkaa huu, ambapo MSD imepata kibali cha kuanza usambazaji.

Aidha, amesema kuna kiwanda cha kuzalisha mipira ya mikono (glove) kilichopo Idofi mkoani Njombe na sasa kina uwezo wa kuzalisha glove 10,000 huku akieleza kiwanda hicho kitaanza uzalishaji Julai 25 na kitakidhi mahitaji kwa asilimia 100.

“Kiwanda kitatoa ajira zaidi ya 200 za moja kwa moja na ambazo si za moja kwa moja. Viwanda vyote hivyo vitaokoa fedha za kigeni na tunataka malighafi za viwanda hivi zitoke nchini. Tukifanikwa tunaweza kutengeneza mzunguko mzima na hivyo kuimarisha uchumi


Meneja kutoka Idara ya Mipango, Tathimini na Ufuatiliaji wa Bohari ya Dawa (MSD) Hassan Ibrahimu akizungumza mbele kwenye Semina ya Wahariri wa Vyombo vya habari nchini kuhusu hatua mbalimbali inazochukua kuondokana na changamoto ya kuagiza vifaa tiba mbalimbali kutoka nje ikiwa pamoja na kuanzisha viwanda viwili vya barokoa na kimoja cha kuzalisha mipira ya mikono (groves).


Meneja Mawasiliano na Uhusiano Bohari ya Dawa (MSD) Etty Kusiluka akitoa maelekezo mbalimbali wakati wa semina ya siku mbili ya Wahariri wa Vyombo habari nchini,  jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF),Deodatus Balile (kulia) pamoja na Meneja Mawasiliano na Uhusiano Bohari ya Dawa (MSD) Etty Kusiluka na baadhi ya Wahariri wakifutilia wasilisho lililokuwa likihusu Mabadiliko ya sheria ya MSD n Uanzishwaji wa kampuni Tanzu.

Mweyekiti wa Muda wa semina ya siku mbili ya Wahariri wa Vyombo habari nchini,Mgaya Kingoba akitoa muongozo namna ya kufanya majadiliano kufuatia mawasilisho yaliyokuwa yakiwasilishwa ukimbini humo.Pichani kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Mavere Tukai akifuatilia.


Baadhi ya Wafanyakazi waandamizi wa Bohari ya Dawa (MSD) wakifuatilia mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiwasilishwa ukumbini humo wakati wa semina ya Wahariri wa Vyombo vya habari ambayo imeratibiwa na Bohari ya Dawa(MSD) jijini Dodoma.







Baadhi ya Wahariri wa Vyombo vya habari wakifuatlia yaliyokuwa yakiendelea kwenye semina hiyo.Picha zote na Michuzi Jr-MICHUZI MEDIA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...