Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Idd kwa Maimamu wa Misikiti, walimu wa Madrasa, Wajane na Yatima Mkoa wa Pwani .
Salaam Hhzo zimewasilishwa leo April 20.2023 na Nickson Simon Mkuu wa Wilaya ya Kibaha kwa Niaba ya Mkuu wa mkoa wa Pwani alhaj Abubakari Kunenge.
Nickson alieleza kati ya vitu vilivyotolewa ni pamoja na mchele,sukari na fedha.
Batuli Mayelo ni Mwakilishi wa wajane alimshukuru Rais kwa alichotoa na kumuombea kwa Allah amlinde katika majukumu yake ya kuliongoza Taifa.
Sheikh Mkuu Mkoani Pwani Hamis Mtupa aliwataka wananchi kuendelea kumuombea Rais na kumuunga mkono kwa makubwa anayoyafanya nchini, kutatua kero za wananchi na kuinua maendeleo na uchumi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...