Dar es Salaam, April 20, 2023
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe Mohammed Mchengerwa na Balozi wa Ujerumani nchini, Regine Hess, leo Dar es Salaam, wameshuhudia kusainiwa kwa Mkataba wa Utekelezaji wa Mradi wa Bilioni 15 (Euro milioni 6), Kusaidia Tanzania Kupambana na Wanyama Waharibifu katika maeneo ya Kusini mwa Tanzania.
Mkataba huo umetiwa saini na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi na Dkt. Mike Falke, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Ujerumani nchini (GIZ).
“Kusainiwa kwa mkataba huu ni ishawa kuwa Serikali imeanza na itaendelea kulipa uzito suala la uhufadhi na hasa kupunguza athari za wanyama waharibifu kama tembo kwa kushirikiana na wadau kama mnavyoona hapa leo,” alisema Waziri Mchengerwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...