Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Dodoma

BOHARI ya Dawa (MSD) imesema ipo katika hatua za mwisho kusajili kampuni tanzu ya kusimamia uzalishaji wa bidhaa ambayo itaendeshwa kibiashara.

Hayo yamesemwa leo Aprili 5, 2023 na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai, wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari nchini ambao wamehudhuria semina ya kuwajengea uwezo na kubadilishana uzoefu inayoendelea jijini Dodoma.

“Katika moja ya eneo ambalo tunasema tumepata mafanikio ni pamoja na uzalishaji bidhaa , na hapa tunasema kwa sauti kubwa.MSD inaviwanda vyake, kiwanda cha Idofi ambacho kinatengeneza glove lakini tunacho , kiwanda cha kutengeneza Maski ambacho kipo Keko.

“Kwenye uzalishaji tulitafakari tukaona tukichukua jukumu kama lilivyo hatutaweza, tukaamua tutafute njia, tukaanzisha kampuni tanzu, tayari iko hatua za usajili na itakuwa inauza bidhaa zake kwa MSD. Tumeiruhusu MSD ijiendeshe kibiashara.
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Mavere Tukai akizungumza leo Aprili 5,2023 jijini Dodoma wakati akifafanua mambo mbalimbali kuhusu Bohari ya Dawa kwenye semina ya siku mbili iliyoanza leo ambayo imeratibiwa na Bohari ya Dawa(MSD) kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini



Baadhi ya Wahariri wa Vyombo vya habari wakifuatlia yaliyokuwa yakiendelea kwenye semina hiyo

Baadhi ya Wafanyakazi waandamizi wa Bohari ya Dawa (MSD) wakifuatilia mambo mbalimbali yaliyokuwa yakielezwa na MSEMAJI Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Gerson Msigwa leo Aprili 5,2023 jijini Dodoma wakati akitoa salamu kwenye semina ya siku mbili iliyoanza leo ambayo imeratibiwa na Bohari ya Dawa(MSD) kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini.
 Mfamasia Mkuu wa Serikali Bw. Daudi Msasi akizungumza leo Aprili 5,2023 jijini Dodoma wakati akifafanua mambo mbalimbali kuhusu usambazaji wa dawa kwenye semina ya Wahariri ya siku mbili iliyoanza leo ambayo imeratibiwa na Bohari ya Dawa(MSD) kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini
Meneja Mawasiliano na Uhusiano Bohari ya Dawa (MSD) Eti Kusiluka akitoa maelekezo mafupi kabla ya kuanza kwa semina ya siku mbili ya  Wahariri wa Vyombo habari nchini leo  Aprili 5,2023 jijini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...