Na Mbaraka Kambona,

Wafugaji wametakiwa kujua kuwa soko la nyama inayozalishwa hapa nchini limefunguka hivyo wajipange kubadilika na kufanya ufugaji wa kibiashara ili waweze kuongeza tija katika uzalishaji.

Rai hiyo ilitolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega wakati wa hafla ya kugawa madume kwa vikundi vya wafugaji iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida Aprili 6, 2023.

"Ndio maana Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi cha Tshs. Milioni 878. 4 kwa ajili ya kununua haya madume bora 366 ili wafugaji tuweze kuboresha mifugo yetu, tuweze kupata ng'ombe wanaoweza kutoa nyama nyingi na kufanya biashara yenye tija kuliko hivi sasa", alisema

Aliongeza kwa kusema kuwa madume hayo yatawawezesha wafugaji kuwa na ng'ombe chotara ambao wanauwezo wa kuzalisha wastani wa kilo 150- 200 za nyama ukilinganisha na uzalishaji wa kilo 80-120 kwa Ng'ombe wa asili.

"Mifugo ni uchumi, na leo nawaambieni nyama ni dili, Rais Samia amefungua milango, wakati huu tunapokea wageni wengi kutoka nje ya nchi wakitaka kufanya biashara ya nyama na nchi yetu", alifafanua Ulega

Naye, Mbunge wa Iramba Mashariki, Francis Mtinga alimshukuru Waziri Ulega kwa kuwezesha wafugaji wa Wilaya ya Mkalama kupata madume Bora 40 huku akimuahidi kuwa watayatumia vizuri madume hayo kuboresha uzalishaji wa mifugo yao.

Halmashauri ambazo zimepata mgao huo ni pamoja na Mkuranga 50, Mvomero 40, Buchosa 46, Chamwino 50, Maswali 50, Chato 50, Msalala 50 na Mkalama 40.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akikagua madume bora ya ng’ombe ambayo aliyagawa kwa vikundi vya wafugaji katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida Aprili 6, 2023

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...