Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amekagua Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kimagai iliyopo Wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma,ambao mpaka sasa ujenzi wake umegharimu zaidi ya Shilingi milioni 14 ambazo zimetokana na Michango mbalimbali ya Wananchi pamoja na Nguvu kazi.

Kwa Mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, amesema lengo la Mradi huo ni Kupunguza Changamoto ya Upatikanaji wa Huduma za Afya kwa Wananchi kwenye Kijiji hicho.

Akiwa kwenye ziara hiyo Juni 15,2023 Wilayani humo,baada ya kukagua ujenzi wa Zahanati, Katibu Mkuu Chongolo akachangia Mifuko 50 ya Saruji ili kuharakisha Ujenzi wa Kituo hicho cha Afya na Kusogeza Huduma karibu kwa Wananchi.

"Kwenye Sekta ya Afya kazi kubwa inafanyika, Serikali inafanya hivyo Sababu inao wajibu wa kumlinda kila raia wa nchi hii ili kuongeza nguvu kazi, lakini kwenye vituo vya Afya kulikuwa na Changamoto ya Vifaa tiba,

lakini tumezungumza na Wahusika Tamisemi, Wizara ya Afya Kupitia MSD kwamba ifikapo mwezi wa Nane hili zoezi la Vifaa tiba liwe limefikia Ukomo wake ili Wananchi waanze kunufaika na Vifaa tiba vilivyoletwa kwenye Vituo vyote vya Afya nchi nzima" amesema Chongolo.

Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu huyo wa CCM Daniel Chongolo ameambatana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema pamoja na Katibu wa NEC Oganaizesheni Issa Haji Gavu.

Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo (kushoto) akishiriki kuchanganya mchanga na saruji ikiwa ni sehemu ya kushiriki ujenzi Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kimagai iliyopo Wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma,ambao mpaka sasa ujenzi wake umegharimu zaidi ya Shilingi milioni 14 ambazo zimetokana na Michango mbalimbali ya Wananchi pamoja na Nguvu kazi.

Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo  (kulia) akitoka kukagua na kushiriki ya ujenzi Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kimagai iliyopo Wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma,ambao mpaka sasa ujenzi wake umegharimu zaidi ya Shilingi milioni 14 ambazo zimetokana na Michango mbalimbali ya Wananchi pamoja na Nguvu kazi.

Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Kimagai wakifurahia ujio wa Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo katika eneo hilo la ujenzi wa Zahanati yao
Sehemu ya meza kuu  ikifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano huo
Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Kimagai wakifurahia ujio wa Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo katika eneo hilo la ujenzi wa Zahanati yao.





Sehemu ya umati wa  Wananchi wa kijiji cha Kimagai wakimsikiliza Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kukagua ujenzi wa Zahanati yao
Muonekano wa juu wa Zahanati ya kijiji cha Kimagai,Mpwapwa inavyoonekana







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...