Tarehe 23 Juni 2023, Serikali ilishuhudia utiaji saini wa mikataba ya utekelezaji kati ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na wawekezaji kwa lengo la kukabiliana na uhaba wa bidhaa muhimu nchini.

Kampuni ya Sukari Kilombero ilisaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wake wa upanuzi unaotekelezwa mkoani Morogoro ambao unahusisha upanuzi wa Kilimo cha Miwa na Kiwanda kwa ajili ya uzalishaji wa sukari.

Baada ya kukamilika, mradi huo utakaogharimu dola za Kimarekani 238.5 milioni, utaleta ajira mpya zipatazo1404 za moja kwa moja na 15,000 ambazo si za moja kwa moja. Baada ya upanuzi, Kampuni itakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 271,000 za sukari na hivyo kupunguza mahitaji ya uagizwaji sukari kutoka nje.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Gilead Teri (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sukari Kilombero, Guy Williams, wakibadilishana mkataba waliosaini kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda hicho.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sukari Kilombero, Guy Williams, akielezea mradi wa upanuzi unaotekelezwa na Kampuni katika hafla ya utiaji saini mikataba ya utekelezaji
Wawakilishi kutoka miradi 10 iliyopewa hadhi ya kimkakati katika picha ya pamoja na Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Dkr Ashatu Kijaji (katikati mbele) pamoja na viongozi wengine wa Wizara na TIC.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...