Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

Ni rasmi Manchester United ya Uingereza imetangaza kuachana na Golikipa wake namba moja, raia wa Hispania, David De Gea kuelekea msimu ujao wa mashindano wa 2023-2024.

De Gea ameachwa na Manchester United, alitua Kikosini hapo akitokea
Atletico Madrid, mwaka 2011, De Gea amedumu Kikosini hapo kwa miaka 12 na alikuwa miongoni mwa Magolikipa bora kuwahi kutokea Man United.

De Gea ameondoka Man United akiwa amecheza michezo 545, akiwa na michezo 190 ambayo hajaruhusu bao (clean sheet).

Kupitia kurasa zake zake za mitandao ya kijamii, David De Gea ameandika: “Nawaaga mashabiki wote wa Manchester United, nashindwa kuandika ujumbe huu!!!.”

“Nawashukuru wote kwa upendo wenu kwa kipindi chote cha miaka 12 nilipokuwa hapa, Man United, tumeshinda mengi tangu alipokuwa Sir Alex Ferguson ambaye alinileta hapa na kunipa nafasi Kikosini. Ni fahari kwangu kucheza kwenye Klabu hii kubwa na maarufu duniani.”

Hata hivyo, Manchester United imehusishwa kumsajili Golikipa wa Kimataifa wa Cameroon, André Onana.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...