Kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni "Lets Move" kauli ambayo inadhamiria kuhamasisha kila mtu kufanya mazoezi kwa ajili ya afya na kuuweka mwili sawa.
Sherehe hiyo itahusisha mbio za taratibu za kilomita 2.5 kwa Watoto chini ya miaka 14 na kilomita 5.0 kwa walio na miaka 15 na kuendelea. Pia itahusisha halaiki yamazoezi (aerobics), breakdance" na mpira wa mezani (Teqball).
Siku ya Olimpiki husherehekewa kila mwaka tarehe 23 Juni, ikiwa kumbukumbu yakuanzishwa kwa Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa hapo tarehe 23 Juni, 1894, Paris nchini Ufaransa.
Imetolewa na Filbert Bayi,
KATIBUMKUU - KAMATI YA OLIMPIKI TANZANIA
Kwa mawasiliano zaidi +255 754 28717
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...