Na. Dennis Gondwe, DODOMA
WANANCHI wa Kata ya Chamwino wajitokeza kushiriki usafi wa Mazingira wa kila Jumamosi kwa lengo la kuweka Mazingira safi yanayowazunguka na kujiepusha magonjwa yanayosababishwa
na uchafu wa Mazingira.
Akiongelea lengo la wananchi wa kata hiyo kufanya usafi wapamoja wa Mazingira, Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kuwa ni kuhakikisha Mazingira ya kata
hiyo yanakuwa safi. “Kata ya Chamwino, usafi ni tabia yetu.
Muitikio wa wananchi kujitokeza kushiriki katika usafi wa pamoja ni mkubwa unaolenga kuweka Mazingira safi. Muitikio huo pia ni utekelezaji wa maagizo ya viongozi wetu kuelekeza tufanye usafi wa Mazingira ili kujihakikishia Mazingira safi na kuepuka magonjwa yanayotokana na uchafu wa Mazingira” alisema Nkelege.
Alisema kuwa usafi ulifanyika katika maeneo mbalimbali ukijumuisha usafi wa mitaro ya maji ya mvua, maeneo ya biashara na maeneo ya makazi. “Maeneo haya ni muhimu kwa
sababu yanatumiwa na wananchi wengi kupata huduma” aliongeza.
Akiongelea mitaa iliyoshiriki zoezi la usafi katika kata hiyo aliitaja kuwa ni Mtaa wa Mwaja, Mailimbili, Sokoine na Nduka, . “Mtaa wa Mwaja usafi wa pamoja ulifanyika katika Shule ya Msingi
Chinangali ukihusisha kuzibua na kuondoa mchanga uliofunika
mitaro. Pia zoezi la kufyeka vichaka vinavyozunguka eleo la shule ili kuwahakikishia wananfunzi na walimu Mazingira safi na salama. Kwa Mtaa wa Mailimbili, usafi wa pamoja ulifanyika
katika korongo ukihusisha kutoa taka ngumu kama makopo, mifuko ya plastiki na kufyeka vichaka na nyasi zilizoota ndani ya korongo” alisema Nkelege.
Mitaa mingine iliyofanya usafi wa pamoja ni Sokoine na Nduka. “Mtaa wa Sokoine, usafi ulifanyika katika mtaro wa barabara ya Sokoine kuelekea Hoteli ya Okaone ukihusisha kutoa taka ngumu
kama makopo na mifuko ya plastiki iliyozagaa ndani ya mtaro. Mtaa wa Nduka usafi wa jumla ulifanyika katika eneo la wazi maarufu kwa Kimbinyiko ukihusisha kufyeka vichaka na nyasi katika eneo hilo” alisema Nkelege.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...