Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

Wachezaji watatu wa Al Hilal SC ya Sudan, Fabrice Ngoma, Ibrahim Imoro na Lamin Jarjou wameshutumiwa na Klabu hiyo kuvunja mikataba yao.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mitandao ya kijamii ya Klabu hiyo, imeeleza kuwa wachezaji hao wamevunja mikataba hiyo bila taratibu na wote watachukuliwa hatua za kisheria.

“Wachezaji wetu, Fabrice Ngoma, Ibrahim Imoro na Lamin Jarjou wamevunja mikataba yao bila sababu. Hatukubaliani na hilo, tutaanza kuwachukulia hatua za kisheria dhidi yao,” imeeleza taarifa ya Klabu hiyo.

Kiungo raia wa DR Congo, Fabrice Ngoma, amehusishwa kusajiliwa na Klabu ya Simba ya Tanzania wakati Mshambuliaji Lamin Jarjou na Mlinzi wa pembeni (kushoto) kutoka Ghana, Ibrahim Imoro haijafahamika wapi wanaelekea.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...