MWIMBAJI wa  Muziki Nchini Marekani- Multtalent Akon ameunagana na mkali wa Afrika Kusini Brown wanatarajia kuachia wimbo wao uitwao  'Enjoy That' hivi karibuni.

Wimbo huu wa kusisimua, utazinduliwa chini ya lebo ya Muziki ya Akon maarufu ya Konvict Kulture na ngoma hii ni msingi wa kuvutia wa EP ijayo inayosubiriwa kwa hamu ya 'Afro Freak' ambayo itakuwa na sauti za kuvutia, midundo isiyozuilika kusikilizika na midundo ya kusisimua inayoongozwa na amapiano "Enjoy That"ambayo ipo tayari kutawala chati za muziki ulimwenguni.

"Kufanya kazi na  mwanamuziki Brown ilikuwa safari ambayo ilituwezesha kuunda kitu cha pekee kwenye ngoma yetu ya 'Enjoy That'. Amesema Akon katika mahojiano aliyofanya hivi karibuni.

 Inajumuisha kiini cha kuishi bila majuto, kuthamini burudani za maisha na kufurahia kila toleo linalotolewa kwa utayarishaji wake mahiri na maneno ya kutia moyo katika wimbo huo unaangazia hali za watu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...