Miss Tanzania 2022 Halima Kopwe kuwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya urembo  ya  dunia  '71st Miss World' yatakayofanyika   Delhi , India tarehe 9 December 2023

Warembo wote akiwemo Halima  watapokelewa tarehe 8 November kwa ajili ya kuanza kambi rasmi ya msahindano kwa muda wa mwezi mmoja  kabla ya fainali

Kama ilivyoutaratibu siku chache kabla ya kuanza safari Miss Tanzania anatarajiwa  kukabidhiwa bendera ya Tanzania ili kuagwa rasmi na Waziri wa Habari Tamaduni Sanaa na Michezo

Mbali na kwenda kushindana Miss Tanzania atatumia fursa hii kutangaza utalii na Taifa la Tanzania katika jukwaa la dunia Watanzania na wadau wote wa sanaa burudani na michezo wakiwemo wanahabari tuungane kumpa nguvu mwakilishi wetu katika mashindano haya makubwa ya dunia.

Kwa habari zaidi na muendelezo wa matukio yanayojiri yatawekwa kwenye ukurasa rasmi wa Miss Tanzania kwenye mitandao ya jamii @misstanzaniaorganisation 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...