Miss Tanzania 2022 Halima Kopwe kuwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya urembo ya dunia '71st Miss World' yatakayofanyika Delhi , India tarehe 9 December 2023
Warembo wote akiwemo Halima watapokelewa tarehe 8 November kwa ajili ya kuanza kambi rasmi ya msahindano kwa muda wa mwezi mmoja kabla ya fainali
Kama ilivyoutaratibu siku chache kabla ya kuanza safari Miss Tanzania anatarajiwa kukabidhiwa bendera ya Tanzania ili kuagwa rasmi na Waziri wa Habari Tamaduni Sanaa na Michezo
Mbali na kwenda kushindana Miss Tanzania atatumia fursa hii kutangaza utalii na Taifa la Tanzania katika jukwaa la dunia Watanzania na wadau wote wa sanaa burudani na michezo wakiwemo wanahabari tuungane kumpa nguvu mwakilishi wetu katika mashindano haya makubwa ya dunia.
Kwa habari zaidi na muendelezo wa matukio yanayojiri yatawekwa kwenye ukurasa rasmi wa Miss Tanzania kwenye mitandao ya jamii @misstanzaniaorganisation

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...