Na John Walter-Ngorongoro

Baadhi ya wananchi wanaoishi ndani ya Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro katika wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha wamepaza sauti zao kupitia vyombo vya habari wakiwa na Mabango yaliyoandikwa jumbe mbalimbali.

Wananchi hao wakiongozwa na kiongozi wa Kimila wa jamii ya Wamasai Laigwanani Petro Tengesi wamefanya maandamano ya amani katika kijiji cha Kapenjiro wakiwa wamebeba mabango yanayoonesha kuchukizwa na wanaopinga wao kuhamia Msomera.

Wamesema wapo tayari kuhama muda wowote na kwamba wameshafika katika eneo la Msomera kujionea hali ilivyo na kwamba wameridhishwa nayo.

Kiongozi huyo wa mila amesema wamechoka kuishi eneo la Ngorongoro kwa kuwa hawana uhuru wa kufanya shughuli yoyote ya maendeleo kikiwemo kilimo ambacho kingewawezesha kupata chakula.












Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...