*Kanisa likijihusisha na siasa litakuwa na ubinafsi wa kupendelea upande mmoja

*Latangaza mkutano kufanyika Dar

Na Chalila Kubuda ,Michuzi TV

Kanisa la Halisi la Mungu Baba limesema katika utoaji huduma ya kiroho haijihusishi na Siasa kwani kufanya hivyo Kanisa  linaweza kuwa na ubinafsi kwa kupendelea chama.

Licha ya kuwa hawajihusishi  waumini wake hawatambuani kwa vyama na kufanya waumini kuwa familia moja  kwa kufuata masuala ya Ki-Mungu.

Hayo aliyasema jijini Dar es Salaam  kiongozi wa Kanisa Halisi la Mungu Baba, Baba Halisi wakati wa kutangaza mkutano utaofanyika Mlimani City Septemba 10 jijini Dar es Salaam utaohudhuriwa na makundi mbalimbali wakiwemo viongozi wa Serikali.

Baba Halisi amesema  Tanzania inatajwa kuwa chanzo cha  baraka kufuatia amani, utulivu na rasilimali za nchi kutokana na uwepo wa uongozi unaozingatia haki.

 alisema  inatakiwa Watanzania kujua jinsi nchi ya Tanzania ilivyobarikiwa na Mwenyezi Mungu kwa kuwa rasilimali za kutosha.

Halisi amesema  Watanzania wajitambue na  kubadilisha mienendo yao  kwa kuhakikisha wanakuwa baraka kwa wengine kutokana na rasilimali zilizopo ambapo mataifa mengine hayana rasilimali hizo.

"Kwa kuwa Tanzania imebarikiwa, Watanzania  wanapaswa kubadilisha mienendo yao kwa kuchangua namna bora ya kuishi ili kuendelea kuwa baraka kwa mataifa mengine," amesema

Halisi alisema kanisa hilo limekuwa likiishi kwa kuhimiza amani, upendo, kuzalisha haki  ndio maana limeandaa mkutano wa kijamii   na utahudhuriwa watu  zaidi ya watu 1000 kutoka ndani na nje ya nchi  watashiriki.

Alisema mkutano huo utabebwa na mada isemayo Tanzania ndiyo chanzo cha baraka kwa mataifa yote lengo ni kuwapa uelewa Watanzania kuzitambua rasilimali zilizopo.

"Kanisa hili ili kuhakikisha rasilimali zinalindwa  ikiwepo amani, upendo  na kuzalisha haki, tumekuwa  na desturi ya kila siku saa 11 asubuhi kuwaombea viongozi waliopo madarakani  wazidi kuongoza kwa haki,"alisema.

Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Halisi la Mungu Baba, Baba Halisi akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mkutano waliouandaa, Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...