Baraza la Kuu la Waislam Mkoa wa wa Dar (BAKWATA) wakiongozwa na Kaimu Sheikh wa Mkoa na Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Mkoa huo Sheikh Walid  Alhad Omary wamejumuika pamoja kutembelea wagonjwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kuwaombea Dua, kuwafariji na kuwapa vitu kadhaa kwa ajili ya matumizi yao.

Ziara hiyo imefanyika leo kuelekea sherehe za mazazi ya Mtume Muhammad (S.A.W) itakayofanyika Kimkoa Septemba 27 mwaka huu katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.

Sheikh Walid amesema katika kuelekea kuazimisha sherehe hizo, BAKWATA Mkoa wa Dar Es Salaam imeandaa shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kufanya mihadhara misikitini, kutembelea wagonjwa na kuwaombea Dua, kuchangia damu, kufanya usafi na kutoa sadaka kwa wagonjwa.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Bw. Aminiel Aligaesha amemshukuru Sheikh Walid pamoja na BAKWATA kutembelea wagonjwa, kuwaombea dua na kutoa sadaka za vitu kwao ikiwemo sabuni, miswaki, dawa za meno, pampasi n.k.

Aligaesha amesema dini ya kweli ni Ile inayowajali wahitaji hivyo walichokifanya ndicho Mwenyezi Mungu anachotaka.

Sheikh Walid ameahidi kuendelea kushirikiana na MNH katika maeneo mbalimbali ya kusaidia wagonjwa waliolazwa ili kutoa mchango  wa kijamii Kwa wahitaji.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...