Na Karama Kenyunko Michuzi Tv

 MWENYEKITI wa Baraza la 12 la Uongozi Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT), Profesa, Ulingeta Mbamba amesema baraza hilo chini kufanya kazi ya uongozi wake, litahakikisha linafanya kazi ya ziada kuhakikisha kiasi kikubwa kllichowekezwa na serikali kwenye miundombinu ya usafirishaji hakipotei bure.

Amesema Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye miundombinu ya usafirishaji, hivyo hata wao hawana budi kufanya kazi ya ziada katika kuhakikisha wanaunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali kwenye sekta ya usafirishaji.

Akizungumza katika hafla ya kuliaga baraza la uongozi la 11 na kukaribisha baraza jipya la uongozi la 12,  leo Septemba 30,2023 chuoni hapo, Mbamba pia amelipongeza Baraza la 11 lililomaliza muda wake kwa kufanya kazi kubwa ambayo Maendeleo yakr yamekuwa yakizidi kuonekana kila siku

Aidha ameishukuru menejimenti ya Chuo cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) kwa kuendelea kufanya vizuri, hivyo baraza lipo kwaajili ya kusaidia na maendeleo yaweze kuonekana zaidi.

Naye, Mjumbe wa Baraza la 11 la Uongozi wa Chuo, Mhandisi Eliona Simbo, akiongea kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza , amesema kwa kipindi walichokuwepo walipata ushirikiano mkubwa na menejimenti ya Chuo hivyo kufanya kuonekana kwa maendeleo chuoni hapo

"Haya maendeleo yanayoonekana, hatuna budi kuishukuru menejimenti ya Chuo kwa ushirikiano mkubwa walioutoa pindi tunapoingia kazini kwa mara ya kwanza hadi kufikia mwisho na kuchaguliwa kwa Baraza lingine". Amesema

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT), Profesa Zacharia Mganilwa amesema uanzishwaji wa Kituo cha Mafunzo ya Usalama Barabarani ambacho kinafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika ni moja ya mafanikio yaliyopatikana katika Uongozi wa Baraza la 12.

" Kutokana na wingi wa matukio ya ajali barabarani, kituo hiki kimedhamiria kupunguza ajali za barabarani". Amesema Profesa Mganilwa.

Mwenyekiti wa Baraza la 12 la Uongozi wa Chuo, Prof. Ulingeta Obadiah Mbamba akizungumza katika hafla ya kuliaga Baraza la Uongozi la 11 lililomaliza muda wake, hafla ambayo imefanyika leo Septemba 30,2023 Jijini Dar es Salaam.
Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi Jipya la 12 Dkt.Dina Zawadi Machuve (kulia) akipokea vitendea kazi kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la 11 lililopita Mhandisi Dkt. Gemma Modu katika hafla ya kuliaga Baraza la Uongozi la 11 lililomaliza muda wake, hafla ambayo imefanyika leo Septemba 30,2023 Jijini Dar es Salaam
Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la 11 lililopita Mhandisi Dkt. Gemma Modu akizungumza katika hafla ya kuliaga Baraza la Uongozi la 11 lililomaliza muda wake, hafla ambayo imefanyika leo Septemba 30,2023 Jijini Dar es SalaamMjumbe wa Baraza la 11 la Uongozi wa Chuo, Mhandisi Eliona Simbo akizungumza katika hafla ya kuliaga Baraza la Uongozi la 11 lililomaliza muda wake, hafla ambayo imefanyika leo Septemba 30,2023 Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT), Prof. Zacharia Mganilwa akizungumza katika hafla ya kuliaga Baraza la Uongozi la 11 lililomaliza muda wake, hafla ambayo imefanyika leo Septemba 30,2023 Jijini Dar es Salaam
Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi Jipya la 12 Dkt.Dina Zawadi Machuve (kulia) akikabidhi zawadi kwa Wajumbe wa Baraza la 11 la Uongozi wa Chuo katika hafla ya kuliaga Baraza la Uongozi la 11 lililomaliza muda wake, hafla ambayo imefanyika leo Septemba 30,2023 Jijini Dar es Salaam
la Uongozi jipya la 12 la Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa hafla ya kuliaga Baraza la Uongozi la 11 lililomaliza muda wake, hafla ambayo imefanyika leo Septemba 30,2023 Jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Baraza la 12 la Uongozi wa Chuo, Prof. Ulingeta Obadiah Mbamba akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la 12 la Uongozi wa Chuo na Baraza la Uongozi la 11 lililomaliza muda wake wakati wa hafla ya kuliaga Baraza hilo leo Septemba 30,2023 Jijini Dar es Salaam
(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO))

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...