Na Mary Margwe, Geita

Naibu Waziri Mkuu na Waziri Mkuu wa Nishati Dotto Mashaka Biteko anatarajia kuwa Mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Maonyesho ya sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini yatakayofunguliwa Septemba 23 Mwaka huu katika Halmashauri ya Mji wa Geita huku Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan akitarajiwa kufunga Maonyesho hayo.

Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Martin Shigelawakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya EPZA vilivyopo katika Kata ya Bombambili Halmashauri ya Mji wa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Martin Shigela amesema,maonyesho ya mwaka huu yamekuwa na mwitikio mkubwa kutoka na kuwepo Kwa washiriki wengi zaidi kujitokeza kuonyesha shughuli wanazozifanya ukilinganisha na Mwaka Jana.

Shigela amesema Mwaka 2018 Mkoa wa Geita ulianzisha Maonyesho ya Teknolojia ya Madini dhamira ikiwa ni wananchi kupata maarifa mapya watakayoyatumia katika shughuli ya uchimbaji wa madini, utafiti, uongezaji thamani, na uchechuaji.

“ Maonyesho haya yalianza 2018 na mwaka huu ni maonyesho ya sita ya madini ambapo dhamira ni kuhakikisha kwamba wananchi wanapata maarifa mapya watakayoyatumia katika shughuli za utafiti,kuongeza thamani na shughuli za uchenjuaji,

Aidha amefafanua kuwa mwaka jana walipata washiriki  250  ukilinganisha na Mwaka huu washiriki walioimgia ni zaidi ya 400, ambapo amesema hiyo ni kutokana na mwitikio mkubwa wa wanachi wachimbaji, Wafanyabiasha hasa makampuni yanayojihusisha  na utafiti wa Madini, yanayojihusisha na uchechuaji, yanayojihusisha na Uchimbaji, yanayojihusisha na Teknolojia ya uongezaji thamani.

Shigela amesema hiyo yote inatokana na kuwepo Kwa uelewa wa maana Maonyesho, kwani wameona umuhimu wa kuja kwenye hayo Maonyesho, hivyo ninvema wananchi hususani wananchi wajimbaji wakajitokeza Kwa wingi ili kuja kujifunza Teknolojia nanmaarifa mapya yatakayoyatoa hapo walipo na kuwapeleka kwenye viwango vingine.

"  Mwaka huu washiriki walioingia mpaka sasa ni zaidi ya 400 maana yake mwitikio ni mkubwa na wananchi hasa wachimbaji wameelewa maana ya uchimbaji hususan makampuni yanayojihusisha na uchimbaji,uchenjuaji ,uongezaji thamani kwa maana kwamba wameona umuhimu wa kushiriki katika maonyesho haya.”amesema Shigela

Aidha amesema Mkoa umeweka mazingira mazuri ili kuwawezesha wadau wa sekta ya madini kuja na teknlojia mpya na rahisi zitakazowawezesha wachimbaji wadogo kufaidika na teknolojia hizo kwa gharama ndogo za uchijimbaji ,uchenjuaji na uongezaji thamani wa madini ili nchi ifikie hatua ya kuhifadhi dhahabu ambayo imeongezwa thamani kwa zaidi ya asilimia 100.

" Sisis kama Mkoa tumeshaweka  Mazingira mazuri ya kwanza  ya kuwapokea makampuni yote yanayojihusisha  na utafitiwa Madini  ili wake na  Teknolojia mpya lakini  Teknolojia rahisi itakayowawezesha  wachimbaji  wetu wadogo kufaidika na  hiyo Teknolojia" amesema Shigela.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa Shigela pia ametuamia nafasi hiyo kuwakaribisha wananchi hasa wanaojishughulisha na uchimbaji,uongezaji thamani na uchenjuaji wa madini kufika katika viwanja hivyo kujifunza na kujionesha mitambo na mshine kwa ajili ya shugfhuli za uchimbaji.
 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...