MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Abdulrahman Kinana, ameziagiza kamati za siasa za CCM, kuwafuatilia na kuwachukulia hatua wanachama walioanza kupitapita kusaka ubunge na udiwani.

Amesema wanaofanya hivyo wanakiuka kanuni, utaratibu na miongozo ya uchaguzi ndani ya CCM.

Amesema kwamba watakaobainika hawatapitishwa na vikao vya maamuzi kugombea nafasi hizo, hata kama wataongoza katika kura za maoni.

Kinana ameyasema hayo leo Septemba 5, 2023, wilayani Hai, Kilimanjaro katika mkutano mkuu wa jimbo la Hai, uliohusu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, jimboni humo.

“Nataka nitumie fursa hii kuziagiza kamati za siasa za CCM nchi nzima, zikisaidiwa na kamati za maadili nchi nzima, kuwafuatilia wale ambao wameanza kuzungukazunguka kutafuta ubunge, udiwani, uenyekiti wa mtaa au kitongoji kuanzia sasa,” ameagiza Makamu Mwenyekiti na kuongeza:

“Hatuna nafasi ya kuhangaishwa na watu wanaotafuta uongozi kipindi hiki, wasubiri hadi mwezi wa saba mwaka 2025, Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) itaamua tarehe ya kwenda kuchukua fomu, kabla ya hapo unavunja kanuni".

Amesema mwana CCM asifikiri kwamba akianza kampeni kabla ya wakati, akapigiwa kura akawa wa kwanza, atapitishwa kugombea, hapana, hatapita.

"...alianza kampeni mapema, alitoa rushwa, alikivuruga Chama, hata upate kura za wajumbe wote hutapita," ameonya Ndugu Kinana.

Amebainisha kwamba, kuna vigezo vingi vinatazamwa zikiwamo; kura, uzingatiaji wa maadili na kanuni.

"Je, ulitoa rushwa, ulizingatia kanuni, uliwachafua viongozi wenzako walioko madarakani? Kwa hiyo unaweza ukawa wa kwanza lakini ukawa wa mwisho,” ametahadharisha.

Aidha amewataka wanaccm wote kushirikiana na viongozi waliochaguliwa ambao wana wajibu wa kutekeleza ahadi zilizotolewa na Chama kwa Watanzania.














 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...