Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la
Polisi Nchini, CP Awadhi Haji akiwasili katika ukumbi wa Polisi Jamii uliopo
mkoani Dodoma alipopokelewa na Maofisa wa Jeshi la Polisi toka Makao Makuu
kabla ya kuanza kikao kazi cha Maofisa wa Mkoa wa Dodoma na Wilaya zake zote.
(PICHA NA JESHI LA POLISI)
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini, CP Awadhi Haji akiteta jambo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi (ACP) Martine Otieno baada ya kumalizika kikao kazi kilichowajumuisha Maofisa wa Mkoa wa Dodoma na wilaya zake.
(PICHA NA JESHI LA POLISI)
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini, CP Awadhi Haji akizungumza na Maofisa wa Mkoa wa Dodoma na Wilaya zake zote (Wapo Pichani) katika kikao kazi chake ambapo aliwataka kuhakikisha wanakabiliana na kutokomeza uhalifu wa aina yoyote katika mkoa huo.
(PICHA NA JESHI LA POLISI)
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi (ACP) Martine Otieno akitoa taarifa fupi ya Mkoa kabla ya kumkaribisha Kamishna wa Operesheni na Mafunzo CP Awadhi katika kikao kazi cha Maofisa wa Mkoa wa Dodoma pamoja na wilaya zake.
(PICHA NA JESHI LA POLISI)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...