Kiongozi
wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa -2023 ndugu Abdullah Shaib Kaim
amezindua Mradi wa Maji wa Kibaoni Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya na
kusema kuwa anaishukru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kwa utekelezaji miradi mingi ya maendeleo ikiwemo miradi wa maji.
Pia, amewashukru wadau ambao wameweza kushirikiana na Serikali kwa kutekeleza mradi wa maji wa Kibaoni.
Mheshimiwa
Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema kuwa mradi huu wa Kibaoni
umejengwa kwa lengo la kuhudumia wananchi wa vijiji viwili vya kibaoni
na Ihani.
Hata
hivyo katika kuhakikisha kuwa mradi huu unakuwa endelevu, wananchi
waendelea kutunza vyanzo vya maji, miundombinu ya maji pamoja na
mazingira kwa ujumla " amesema.
Sambamba
na kuzindua kwa mradi huo, Mwenge wa uhuru wa Kitaifa-2023 umeweza
kutembelea chanzo cha maji cha Itamboleo pamoja na kupanda miti rafiki
kwa mazingira ili kuweza kuhifadhi na kulinda chanzo cha maji cha
Itamboleo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...