Na Mwandishi Wetu, Nanyumbu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amepokelewa na maelfu ya wananchi wa Nanyumbu Mkoani Mtwara waliosimama barabarani kumsikiliza na kumsalimia.

Rais Samia ameendelea kupokelewa kwa kishindo na wananchi wa mikoa ya Mtwara na Lindi katika ziara yake ya mikoa hii ya kusini.

Kila msafara wake unapopita, maelfu kwa maelfu ya wananchi wamejitokeza kumlaki, kumsikiliza na kumshangilia kutokana na maendeleo makubwa ambayo serikali yake imeleta kwenye mikoa ya kusini ndani ya miaka miwili tu.

Sekta za kilimo, miundombinu, umeme, maji, elimu na afya ni miongoni mwa maeneo ambayo yameshuhudia uwekezaji mkubwa wa serikali chini ya utawala wa Rais Samia kwenye Kanda ya Kusini na kwingine nchini.

Akizungumza na wananchi hao leo wilaya za Nanyumbu na Masasi, Rais Dkt. Samia ametoa wito kwa wananchi kufanya kazi kwa bidii.

Katika ziara hiyo Rais Dkt. Samia amepata wasaa wa kusikiliza changamoto mbalimbali za wananchi na kutoa nafasi kwa wawaziri wa sekta husika kutolea ufafanuzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...