Na Nasra Ismail, Geita
Mamlaka ya Udhibiti wa nishati na maji EWURA imetunga sheria mpya na ambayo itamruhusu mtu yoyote kujenga kituo cha mafuta maeneo ya vijijini na kuuza kwa bei elekezi ili kuachana na mafuta ya kupima kwenye machupa(mabobo).
Akizungumza na taasisi za nishati katika Kongamano katika maonesho ya 6 ya madini mjini Geita meneja wa EWURA kanda ya ziwa George Mhina alisema sheria ya sasa itamruhusu MTU yoyote kujenga kituo cha mafuta.
Mhina aliongeza kuwa MTU ataruhusiwa kujenga kituo cha mafuta kwa ghalama za chini kuanzia mil 50 ili kuondokana na kununua mafuta kwa kupima kwenye vichupa.
Aidha mhina aliwahamasisha wananchi kuchangamkia fursa ya ujenzi wa vituo hivyo ili waweze kuuza mafuta kwa bei elekezi.
"Wananchi changamkieni fursa ya ujenzi wa vituo bibi ili kutokomeza uuzwaji wa mafuta kwenye maeneo yasiyo rasmi haswa barabani na kwenye madumu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...