Na Humphrey Shao,Michuzi TV

Mwenyekiti wa bodi ya REA na TAWENI ,Mh Janet Mbene ametoa wito kwa wanawake wa Kigamboni kuacha kutumia mkaa na kuni na waanze kutumia Gesi na Mkaa mbadala hili kuweza kulinda mazingira.

MH Mbene amesema hayo leo jijini Dar es Salaam  katika Wilaya ya Kigamboni wakati alipokuwa akizungumza na wanawake wajasilimali wa Wilaya  hiyo.

"Matumizi ya mkaa mbadala ayaepukiki Kwani tunavyoendelea kutumia mkaa unaokatwa kwenye miti tunachangia sana kwa kiasi kikubwa kufanya uharibifu wa mazingira na kupelekea kuapata mabadiriko ya Tabia nchi" amesema Mh Mbene.

Ameongeza kuwa Matumizi ya kuni pia uchangia matatizo makubwa ya kiafya ikiwemo wanawake na Wasichana  kupata tatizo la kutoa mimba na homa ya mapafu.

Ametaja kuwa Taweni imejipanga katika kumkomboa Mwanamke  kiuchumi  kwa kupitia vikundi hili waweze kuacha kutumia mkaa na kuni na waanze kutumia Gesi na mkaa Mbadala.

Ameongeza  kuwa  ni muda sasa wa kinamama kujifunza namna ya kubadilisha maisha kwa kujifunza kutumia Nishati mbadala hivyo wamama waache kujifunza kwani kujifunza ndio kila kitu.

 

 Mwenyekiti wa bodi ya REA na Taweni Mh Janet Mbene Mbene akizungumza na wanawake wa KIGAMBONI ambao waliofika katika semina ya Matumizi ya Nishati Mbadala.

Mwenyekiti wa bodi ya REA na Taweni Mh Janet Mbene  akionja moja ya chakula kilichopikwa na Nishati mbadala.
Mwenyekiti wa bodi ya REA na Taweni Mh Janet Mbene  akisindikizwa na wanawake wa Kigamboni  kwenda jukwaani
Mkurugenzi Mtendaji wa Taweni Florance Masunga akizungumza na wanawake wa Wilaya ya Kigamboni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...