Na Nasra Ismail, GEITA

 jumla ya sh milioni 749  zinatumika kujenga shule mpya sekondari ya Mkungo iliyopo Chato mkoani Geita ikiwa ni miongoni mwa moja ya miradi mingi inayoendelea kufanywa na mfuko wa maendeleo ya jamii Tasaf mkoa wa Geita ambayo itarahisishia watoto kutembea umbali mdogo kufata elimu.

Mradi huo ambao utafanikisha ujenzi wa jengo la utawala, nyumba za walimu 2, kisima cha maji, matundu 28 ya vyoo pamoja na maktaba utasaidia maendeleo makubwa ya elimu katika kijiji cha Mkungo.

 Akitembelea mradi huo Waziri  wa nchi Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala bora George Simbachawene aliwapongeza TASAF  kwa kufanikisha mradi huo ambapo mpaka sasa pesa iliyotumika ni ndogo ukilinganisha na ubora wa majengo unavyoonekana.

Aidha alimpongeza mbunge wa Chato Medard Kalemani kwa kufanikicha maendeleo ya katika jimbo hilo hasa katika sekta ya elimu ambapo katika kipindi cha miaka mitatu zimejengwa shule 19.

Simbachawene aliongeza kuwa shule hii itawasaidia watoto kupata elimu kwa urahisi zaidi ambapo mwanzo iliwalazimu kutembea umbali mrefu kufata shule.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...