Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt. Erasmus Kipesha amewataka watumishi wa Mamlaka hiyo kufanya kazi kwa bidi, ubunifu na kuongeza tija ili kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria.

Dkt. Kipesha ametoa kauli hiyo leo Mkoani Dar es Salaam katika ofisi ndogo za TEA mara baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Septemba 23, 2023 kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo.

Aidha, amewasisitiza watumishi wa Mamlaka hiyo kuwa, nia na matarajio ya Mhe. Rais ni kuona TEA ikitekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria lakini pia kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Tawala. Hayo yote yanawezekana endapo kila mtumishi ataongeza bidi, kujituma na kuongeza tija katika utekelezaji wa majukumu yake.

‘‘Naamini kila mtumishi anajua kuwa kazi kubwa ya TEA ni kutafuta vyanzo mbalimbali vya mapato ili kusaidia jitihada za Serikali za kuboresha miundombinu ya Elimu hapa nchini, hivyo kila mmoja ni lazima aweke bidii na ubunifu kwenye hili eneo ili TEA ifikie malengo yake, amesema Dkt. Kipesha’’

Nae Kaimu Mkurugenzi wa Miradi na Utafutaji Rasilimali Bw. Masozi Nyirenda akiongea kwa niaba ya watumishi amesema, Mhe. Rais amempeleka mtu sahihi TEA kwani anaijua taasisi vya kutosha na ana uzoefu kwenye uongozi hivyo ana amini kwamba ataleta mabadiliko chanya ndani ya Mamlaka hiyo.

Ameongeza kuwa, watumishi wako tayari kushirikiana nae kwenye kila hatua na kutembea nae katika safari ya kusimamia na kutekeleza Mpango Mkakati wa TEA wa miaka mitano kuanzia mwaka 2021/2022 hadi mwaka 2025/2026 pamoja na Ilani ya Chama kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa Umma.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...