Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

Tanzania imeweka rekodi ya kufuzu mashindano ya AFCON mara ya tatu baada ya mwaka huu wa 2023 kufuzu ugenini kwenye uwanja wa Annaba nchini Algeria baada ya sare ya 0-0 dhidi ya wenyeji hao Algeria hivyo kufikia alama nane zilizoivusha.

Mara ya kwanza, Tanzania ilifuzu mashindano hayo mwaka 1980 nchini Nigeria, wakati huo Taifa Stars ilikuwa chini ya Kocha Mkuu Joel Bendera. Mwaka 2019 Taifa Stars ilifuzu mashindano hayo ya AFCON nchini Misri chini ya Kocha Emmanuel Amunike.

Mara ya tatu kwenye uwanja wa Annaba, Algeria baada ya kuwalazimisha sare ya 0-0 wenyeji ikiwa ni mchezo wa Kundi F la kuwania kufuzu mashindano hayo. Uganda (The Cranes) wameshindwa kufuzu mashindano hayo licha ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Niger kwenye uwanja wa Marrakech, Morocco.

Katika Kundi hilo F, Algeria walishakata tiketi ya kufuzu mashindano hayo baada ya kuwa na alama 15 baada ya sare dhidi ya Stars (Tanzania) walifika alama 16, wakiwa kwenye nafasi ya kwanza. Stars wamemaliza nafasi ya pili wakiwa na alama nane, huku Uganda wakiwa na alama saba na Niger alama mbili pekee.

Taifa Stars watacheza mashindano hayo yanayoitwa AFCON 2023 ijapokuwa yatafanyika kati ya Januari na Februari 2024 nchini Ivory Coast.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...