Shirika la Viwango Tanzania (TBS ) limeshiriki katika maonesho ya 20 ya Wahandisi Jijini Dar es salaam, katika maonesho haya Shirika limepata nafasi ya kutoa elimu kwa wajasiriamali,wazalishaji wa bidhaa na Wahandisi.

Akizungumza katika maonesho haya Afisa Masoko TBS, Bi. Rhoda Mayungu ametoa wito kwa wahandisi kushiriki katika mchakato wa uandaaji wa viwango katika sekta mbalimbali kwa kutoa maoni na mapendekezo pale kiwango kinapowasilishwa kwa umma ili kupata maoni kabla ya kuhitimishwa, kwani wahandisi ni wadau muhimu.

"Shirika linapoandaa Viwango kabla ya kuhitimishwa hupelekwa kwa umma ili kupata maoni na mapendekezo endapo wahandisi watashirki kikamilifu katika hatua hii itasaidia wananchi kwani wao ni wadau muhimu sana” Alisema

Mmoja wa Wahandisi kutoka shirika hilo Bi. Christina John,amesema"Tupo hapa kwa ajili ya kuwaasa Wahandisi wenzetu ambao wana miradi ya kihandisi, Wahandisi wa majengo, mitambo,kemikali na wengine wote kwa ujumla wanapokua wanafanya miradi wahakikishe vifaa wanavyo tumia vimehakikiwa kwa ubora kwa ajili ya ubora wa miradi hiyo"Alisema

"Tunawaomba Wahandisi wanapotumia vifaa kwenye miradi yao wahakikishe wanatumia vifaa vilivyo thibitishwa na TBS,amewaomba wale ambao hawatumii vifaa vilivyothibitishwa,kulingana na sheria za Viwango wale wanao kiuka taratibu za ubora sheria zitatumika".Alisema






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...