Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania- TPA imekabidhi vifaa Tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 30 vikiwemoVitanda vya kujifungulia wakina mama ( Delivery Beds) 15 kwa Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara -Ligula.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa leo Septemba 9,2023 na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mhe. Juma Kijavara ambaye amemuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TPA ambapo amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Miaka 18 tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania - TPA.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa tunakuahidi sisi kama wana TPA tutaendelea kuunga mkono juhudi zako kama unavyotuunga mkono kwenye shughuli zetu za kila siku na tutakuwa bega kwa bega na wewe.” Amesema Mha. Kijavara

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Ahmed Abbas ameipongeza TPA kwa kurejesha kwa Jamii faida wanayopata na kutoa vifaa tiba hivyo kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara- Ligula.

Aidha Mhe. Kanali Abbas ameipongeza Bandari ya Mtwara kwa kupiga hatua kubwa katika kuhudumia Shehena ya mzigo mbalimbali.

“ Bandari ya Mtwara imepiga hatua kubwa katika kuhudumia Shehena ambapo katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia 2022-2023 imehudumia Shehena zaidi ya Tani Milioni 1.6 na kuvuka lengo la Kuhudumia Shehena Tani Laki nne walilokuwa wamejiwekea.” Amesema Kanali Abbas

Akitoa neno la shukurani baada ya kupokea Vifaa tiba hivyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara- Ligula Dkt. Lobikieki Kisambu, ameushukuru uongozi wa TPA kwa msaada huo ambao unakwenda kuboresha huduma za Mama na Mtoto katika Hospitali hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...