Mkazi wa Kata ya Nala katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma akiwa mwenye furaha akionesha kidole chake cha shahada kilichotiwa wino baada ya kupiga kura kuchagua Diwani wa Kata hiyo katika Uchaguzi mgogo unaofanyika Leo Septemba 19,2023 katika Kata hiyo. Aidha wananchi wa Jimbo la Mbarali na Kata zingine sita wanapiga kura kuchagua viongozi wao.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo tarehe 19 Septemba, 2023 ametembelea na kukagua zoezi la kupiga kura kwenye Jimbo la Mbarali lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo tarehe 19 Septemba, 2023 ametembelea na kukagua zoezi la kupiga kura kwenye Jimbo la Mbarali lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele leo tarehe 19 Septemba, 2023 ametembelea na kukagua zoezi la kupiga kura kwenye Jimbo la Mbarali lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.

Jaji Mwambegele baada ya kutembelea vituo amesema ameridhishwa na utendaji wa Wasimamizi wa Uchaguzi huo na kuongeza kwamba vituo vimefunguliwa kwa wakati na zoezi linaendelea vizuri kwa utulivu na amani.

Aidha, Jaji Mwambegele amezungumza na mawakala wa vyama vya siasa ambao wamemueleza kuridhishwa na mwenendo wa zoezi la kupiga kura na kwamba hakuna changamoto yoyote iliyojitokeza.

Uchaguzi wa Jimbo la Mbarali unafanyika sambamba na kata sita za Tanzania Bara. Kata zenye uchaguzi ni Nala iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mfaranyaki iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Songea, Mwaniko iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Old Moshi Magharibi iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Marangu Kitowo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Rombo na Mtyangimbole iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.
Wananchi wa Jimbo la Mbaràli wakiwa Leo wamejitokeza kupiga Kura kuchagua Mbunge wa Jimbo hilo.

Wananchi wa Jimbo la Mbaràli wakiwa Leo wamejitokeza kupiga Kura kuchagua Mbunge wa Jimbo hilo.
Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mwanaisha Kwariko akikagua vituo vya kura wakati wananchi wa Kata ya Nala iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakipiga kura kuchagua Diwani wao Leo Septemba 19,2023.


Wananchi wamejitokeza kwa wingi kupiga Kura.

Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mwanaisha Kwariko akikagua vituo vya kura wakati wananchi wa Kata ya Nala iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakipiga kura kuchagua Diwani wao Leo Septemba 19,2023.

Mpiga Kura akipakwa wino baada ya kupiga kura.

Wananchi wakiwa kituoni
Karani muongozaji akihakiki jina la Mpiga kuraWananchi waliona umri mkubwa au wagonja walipewa kipaumbele.
Mpiga Kura mwenye mahitaji maalum akisaidiwa kuingia katika kituo cha kupigia kura ili aweze kutimiza haki yake ya kumchagua Kiongozi anayemtaka katika kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya Kata Na.2, katika Kata ya Mfaranyaki Halmashauri ya Manispaa ya Songea, leo tarehe 19/09/2023.

Zoezi la kupiga kura likiendelea Kwa amani na utulivu katika vituo mbalimbali katika Kata ya Mwaniko iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Leo tarehe 19 Septemba, 2023

Wapiga kura wakiendelea kujitokeza kwenye vituo vya kupiga kura kwenye maeneo mbalimbali ya Kata ya Old Moshi Magharibi kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata hiyo iliyopo Halmashauri ya Moshi mkoani Kilimanjaro unaofanyika leo tarehe 19 Septemba, 2023.
Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mh.Jaji Asina Omari akitembelea na kukagua upigaji kura katika Kata ya Marangu Kitowo katika Halmashauri ya Rombo.

Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mh.Jaji Asina Omari akitembelea na kukagua upigaji kura katika Kata ya Marangu Kitowo katika Halmashauri ya Rombo.
Mjumbe wa Tume, Mhe. Magdalena Rwebangira akikagua vituo vya kupiga Kura katika Kata ya Mfaranyaki Halmashauri ya Manispaa ya Songea tarehe 19 September siku ya Uchaguzi Mdogo wa Udiwani.
90

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...