![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2023/09/1-5-1024x643.jpg)
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2023/09/2-8-1024x733.jpg)
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2023/09/3-11-1024x683.jpg)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Mhandisi Cyprian Luhemeja (wa kwanza kulia) na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Leonard Mchau (katikati) baada ya kuwasili katika ofisi hiyo leo septemba 4, 2023 katika mji wa serikali Mtumba jijini Dodoma.
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2023/09/4-10-1024x683.jpg)
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2023/09/292bc102-0bda-482c-874e-5204aab304b0-1024x682.jpg)
![](https://fullshangweblog.co.tz/wp-content/uploads/2023/09/c28b5fcf-e3f2-49e2-82a1-d2ec76670366-1024x682.jpg)
Na.Mwandishi Wetu-DODOMA
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu-kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu Mhandisi Cyprian John Luhemeja amewasili katika Ofisi hiyo Jijini Dodoma Septemba 4, 2023 na kupokelewa na Menejimenti pamoja na watumishi wa Ofisi hiyo, ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu alipoteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan.
Aidha, Katibu Mkuu Luhemeja alikutana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi pamoja na Menejimenti ya Wizara hiyo.
Baada ya mapokezi hayo Mhandisi Luhemeja alikagua maendeleo ya ujenzi wa Ofisi hiyo inayojengwa katika Mji wa Serikali Mtumba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...