Waziri mpya wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki, na Naibu wake Mhe. Dunstan Kitandula leo Septemba 5,2023 wamepitishwa katika mikakati mbalimbali ya kisekta.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi, ndiye aliyoiongoza  Menejimenti ya  Wizara kuwapitisha viongozi hao Wakuu waliokabidhiwa ofisi zao   Jana mtumba jijini  Dodoma.

Katika kikao hicho wakuu wote  wa Idara walihudhuria na kuwasilisha  Mawasiliano kadhaa.

 Akiwakaribisha viongozi hao katika kikao kazi hicho Dkt. Abbasi amefafanua kuwa Wizara hiyo inayochangia asilimia 21 ya Pato la Taifa na 25 ya Fedha za Kigeni ina mikakati mbalimbali ya kuongeza mapato la muhimu ni uwekezaji zaidi katika uendelezaji na utangazaji wa utalii.

Mhe. Kairuki ameteuliwa katika  Wizara hii akitokea Wizara ya TAMISEMI wakati Mhe. Kitandula amekuwa Mbunge.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...