Waziri wa Madini Anthony Mavunde (Kushoto), akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Biashara wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), na Msimamizi Mkuu wa Kliniki ya Biashara katika Maonesho ya sita ya Teknolojia ya Madini, Bi. Samirah Mohamed (kulia), kuhusu Kliniki ya Biashara inayoratibiwa na Taasisi hiyo, kwenye Maonesho ya sita ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika kwenye viwanja vya EPZ Bombambili Mkoani Geita, leo Septemba 29,2023.

TANTRADE imeshiriki Maonesho hayo ikisimamia Kliniki ya Biashara yenye jukumu la kutoa huduma kwa pamoja kusikiliza na kutatua changamoto za wadau na wananchi mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara.

(PICHA NA: HUGHES DUGILO)

Afisa Biashara wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), na Msimamizi Mkuu wa Kliniki ya Biashara katika Maonesho ya sita ya Teknolojia ya Madini, Bi. Samirah Mohamed (kulia), na Bi. Clara Mwamba (Kushoto), Afisa Biashara kutoka katika Taasisi hiyo, , wakiwa katika picha ya pamoja kwenye Banda lao inapofanyika Kliniki ya Biashara kwenye Maonesho ya sita ya Teknolojia ya Madini Mkoani Geita.

Afisa Biashara wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), na Msimamizi Mkuu wa Kliniki ya Biashara katika Maonesho ya sita ya Teknolojia Katika Dekta ya Madini Bi. Samirah Mohamed (wa kwanza kulia), akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Taasisi wezeshi za Serikali zilizoshiriki kwenye Kliniki hiyo katika Maonesho hayo, Geita.

Muonekano wa Banda ya Kliniki ya Biashara katika Maonesho ya Madini Geita.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...