Na Mwandishi Wetu, Mtwara

NAIBU Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile amesema Serikali inatarajia kujenga Bandari mpya katika eneo la Kisiwa Mgao mkoani Mtwara.

Akizungumza mkoani Mtwara wakati wa ziara yake Naibu Waziri Kihenzile amesema hayo jana Oktoba 4 wakati  akikagua utendaji kazi wa Bandari na Kiwanja cha Ndege cha Mtwara.

Naibu Waziri  Kihenzile amesema, bandari hiyo mpya itakuwa ni maalumu kwa ajili ya usafirishaji bidhaa zijulikanazo kama ‘bidhaa chafu’ ambazo ni kama makaa ya mawe na saruji.

Amesema wizara ina mipango ya muda mfupi na mrefu katika usimamizi na matumizi ya bandari ya Mtwara, hivyo moja ya mipango yao ni kujenga bandari mpya wa Kisiwa Mgao.  

"Serikali inakwenda kujenga bandari nyingine mkoani Mtwara katika eneo linalofahamika kama Kisiwa Mgao ambapo kwa sasa hatua za manunuzi zimeanza," amesema.  

Amesema Wizara ya Uchukuzi  inaendelea kuweka mikakati ya namna ya kuimarisha bandari ya Mtwara, ili kuhakikisha bidhaa nyingine pia zinasafirishwa kwa wingi.  



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...