Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mipango, Masoko na Habari kutoka Wakala Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Bw. Prosper Haule akitoa elimu kwa wadau wa Mifugo waliotembelea banda la TVLA kujifunza kazi zinazofanywa na TVLA pamoja matumizi sahihi ya chanjo za Mifugo zinazozalishwa na TVLA kwenye maonesho ya pili ya Kilimo Biashara na Kilimo Marathon 2023 yanayofanyika Gairo Kata ya Chakwale Mnadani Mkoa wa Morogoro Oktoba 13, 2023. Kulia kwake ni Mtaalamu wa TVLA kituo cha Dodoma Bw. Anastasius Ngatata
Meneja wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania-TVLA Kanda ya Kati Dodoma Dkt. Japhet Nkangaga (mwenye miwani) akitoa elimu kwa wadau wa Mifugo waliotembelea banda la TVLA kujifunza kazi zinazofanywa na TVLA pamoja matumizi sahihi ya chanjo za Mifugo zinazozalishwa na TVLA kwenye maonesho ya pili ya Kilimo ni Biashara Kilimo Marathon 2023 yanayofanyika Gairo Kata ya Chakwale Mnadani Mkoa wa Morogoro Oktoba 13, 2023. Kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mipango, Masoko na Habari wa TVLA Bw. Prosper Haule.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo Bi. Sharifa Y. Nabalangana (Kushoto) akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kujifunza kazi mbalimbali zinazofanywa na Wakala kwenye maonesho ya pili ya Kilimo Biashara na Kilimo Marathon 2023 yanayofanyika Gairo Kata ya Chakwale Mnadani Mkoa wa Morogoro Oktoba 13, 2023. Waliosimama kutoka kulia ni Meneja wa TVLA Kanda ya Kati Dodoma Dkt. Japhet Nkangaga na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mipango, Masoko na Habari wa TVLA Bw. Prosper Haule.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabiri O. Makame (kulia) akipata maelezo kuhusiana na matumizi sahihi ya aina 7 za Chanjo zinazozalishwa na Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania-TVLA kutoka kwa Meneja wa TVLA Kanda ya Kati Dodoma Dkt. Japhet Nkangaga alipotembelea banda la TVLA kujifunza kazi mbalimbali zinazofanywa na Wakala kwenye maonesho ya pili ya Kilimo Biashara na Kilimo Marathon 2023 yanayofanyika Gairo Kata ya Chakwale Mnadani Mkoa wa Morogoro Oktoba 13, 2023.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...