MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu amekabidhi matofali 1,250 yenye thamani ya Shilingi Milioni mbili ikiwa ni jitihada zake za kuunga mkono wananchi wa vitongoji vya Ikugha na Daghusa zake uanzisha shule ili kuondoa adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu.

Akikabidhi matofali hayo ,Mtaturu amesema hizo ni jitihada zake za kusaidiana na serikali katikak uhakikisha wanafunzi wanapata mazingira mazuri ya kusomea.

“Niombe Mkurugenzi atuletee mhandisi hapa kwa ajili ya kuchimba msingi haraka na mimi nitatanguliza mifuko 10 ya saruji ,Mwenyekiti unajua nahangaika na nini,nahangaika na matomaso ambao wao hawaamini mpaka waguse au waone,

“Hao watu wapo na wanatuchelewesha sana kufika tunapotaka kufika,wao wanategemea shule imwagwe hapa ikiwa imekamilika hapana lazima ianze na msingi, hivyo mimi nashughulika na matomaso,”amesema Mtaturu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...