Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (Mb.) amewahamasisha wawekezaji wa Tanzania kuendelea kutumia fursa za uwekezaji na biashara zinazojitokeza kutokana na utekelezaji wa sera ya demkorasia ya uchumi.

Ameyasema hayo leo tarehe 08 Oktoba, 2023 nchini India alipokutana na sekta binafsi ya Tanzania jijini New Delhi ikiwa ni siku moja kabla ya kufanyika kwa Kongamano la biashara kati ya Tanzania na India

Kongamano hilo litafunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, linatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 250 kutoka sekta binafsi za India na Tanzania.

Mheshimiwa Waziri Mkumbo, amewahamasisha wawekezaji wa Tanzania kutumia ipasavyo ushirikiano na uhusiano wa kihistoria iliopo kati ya India na Tanzania.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...