Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Alhajj Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema kazi za Misikiti ukiacha kufanya ibada ya sala pia wana jukumu la kutatua changamoto zinazoikabili jamii pamoja na kufundisha Dini kwa vijana.

Amesema Serikali ina wajibu wa kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazofanywa na Misikiti hiyo.

Rais Alhajj Dkt.Mwinyi amesema hayo alipoufungua Msikiti Sheikha Naema Bint Mohamed Al qasimi na kujumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika ibada ya Sala ya Ijumaa Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe :29 Disemba 2023.

Aidha, Rais Dkt.Mwinyi amewashukuru wafadhili familia ya Sheikha Naema Bint Mohamed Al qasimi kwa kujenga Msikiti na Madrasa zake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...