Na.Khadija Seif Michuziblog
NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'Mwana FA' ametoa maagizo matatu kwa Kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha (Tamriso).
Maagizo hayo ni kutoa elimu kwa wasanii wa muziki, wakusanyaji na wanaokusanyiwa mirabaha kabla ya kuanza zoezi la ukusanyaji mirabaha January 14 mwakani.
Akizungumza Leo Disemba 19,2023 alipofanya ziara katika ofisi ya Tamriso Mikocheni Jijini Dar es Salaam,amesema kabla ya ugawaji wa mirabaha elimu inatakiwa kutolewa kwa watu hao wawili, waweze kufahamu na kuepuka malalamiko.
Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kufanyia kazi changamoto mbalimbali ambazo wameziwasilisha kwake na ambazo zimekuwa zikiwasilishwa mara kwa mara.
"Ziara yangu katika ofisi ya Tamriso kwa lengo kujadiliana namna kazi ya kusanyaji wa mirabaha."
Amefafanua kuwa muda si mrefu wasanii wataenda kunufaika kutokana na kazi zao.
Mwenyekiti wa Tamriso, Jane Gonsalves amesema watahakikisha wanazingatia maagizo waliyopewa na Naibu Waziri kwa lengo kufanya vizuri katika ukusanyaji wa mirabaha.
"Utoaji wa elimu kwa wasanii, wakusanyaji wa mirabaha na wanaokusanyiwa utafanyika na utakuwa utakuwa endelevu kufanyika.''
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...