Na. Abel Paul,Jeshi la Polisi-Longido.

Jeshi la Polisi Wilaya ya Longido limeendelea kutoa elimu ya ukatili wa kijinsia makundi mbalimbali ya jamii za kifugaji huku wakitumia siku 16 za kupinga vitendo hivyo kuchangia damu katika kituo cha Afya Longido.

Akiongea mara baada ya zoezi hilo Mkuu wa Polisi wilaya ya Longido Mrakibu mwandamizi wa Polisi SSP Leah Ncheyeki amesema kuwa wilaya hiyo kiasili ni jamii ya kifugaji ambayo imekuwa ikiendelea kuziishi tamaduni ambazo baadhi zimekuwa zikiwanyima fursa hususani watoto wakike wa jamii za kifugaji.

Ameongeza kuwa Jeshi la Polisi wilaya hiyo kupitia siku kumi na sita za kupinga ukatili waliona vyema waendelee kutoa elimu kwa jamii hizo za kifugaji ili kuachana na tamaduni ambazo hazina tija kipindi hiki cha mabadiliko ya dunia.

Aidha amebainisha kuwa wataendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya jamii hizo za kifugaji ili waondokane na vitendo hivyo vinavyowanyima fursa ya kufanya maamuzi.

Kwa upande wake kaimu afisa Tarafa Longido Enna Mtera licha ya kulipongeza Jeshi la Polisi kwa kuanzisha mpango wa Polisi kata ambao umesaidia sana kutoa elimu na kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii hiyo amesema jamii hiyo imekuwa ikiendekeza mila ambazo zinamnyima haki mwanamke na watoto kwa kufanya maamuzi huku akiwaomba Jeshi hilo waendele kutoa elimu zaidi ili kuikomboa jamii hiyo na mila Potofu.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...