Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na timu kutoka Wizara ya Afya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga wametembelea eneo lililoathirika na maporomoko ya matope yaliyopelekea vifo vya watu 89 na majeruhi 139 Wilaya ya Hanang Mkoni Manyara.

Katika ziara hiyo Waziri Ummy amebainisha mambo kadhaa yatakayoendelea kutekelezwa na Serikali ikiwemo kupeleka magari Matatu ya kubebea wagonjwa (Ambulance), kujenga kituo cha Afya katika eneo lililotengwa na Serikali kwa makazi ya watu.

“Serikali itaendelea kuwahudumia majeruhi waliobakia kwa sasa ambao ni Watano kwa gharama za Serikali Kama alivyoelekeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.” Amesema Waziri Ummy.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...