Waziri wa Maji Mhe Jumaa Aweso amefanya mabadiliko ya Kiuongozi katika Mamlaka ya Maji Utete kwa kumuondoa kwenye nafasi yake Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo bwana Christopher Mwigune akiwa wilayani Rufiji alipofanya kikao maalum cha kuongea na Watumishi wa Sekta ya Maji wilaya ya Rufiji na wilaya jirani za mkoa wa Pwani.

Awali pia Waziri Aweso alifanya mabadiliko ya kiutendaji eneo la Maji Vijijini (RUWASA) kwa mabadiliko ya Meneja wa Wilaya hivyo;

Katika hatua nyingine, Waziri Aweso amemtambulisha rasmi kwa uongozi wa serikali ya Mkoa na Wilaya Meneja mpya wa wilaya wa Maji Vijijini (RUWASA) Eng Alkam Omari Sabuni na kumuelekeza pia Kukamimu nafasi ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Utete katika kipindi hiki cha Mpito ambacho ataifanya mabadiliko makubwa mamlaka hiyo na kuiunda upya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...